Ushairi wa Abdilatif Abdalla Katika Kubainisha Utamaduni wa Waswahili
Date
2018
Authors
Maitaria, Joseph Nyehita
Wafula, Richard Makhanu
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Journal of Linguistics and Language in Education
Abstract
Makala haya yanafafanua maudhui yaliyomo katika tungo za mashairi
ya Abdilatif Abdalla kwa kuzingatia namna masuala ya utamaduni
waWaswahili yanavyowasilishwa. Masuala hayo yanahusu namna
wenyeji hao wanavyotangamana na wanavyoshughulikia maisha yao
kwa ujumla. Kadhalika, ubainishaji wa vipengele hivyo
vimewasilishwa kwa kuzingatia taijriba ya mtunzi kama mmoja katika
jamii hiyo. Mashairi hayo yanapozingatiwa, inabainika kuwa; hisi za
mtunzi zimedhibitiwa kwa lugha teule ya mafumbo inayojikita katika
zaidi katika ‘lugha’ au ‘lafudhi’ yake ambayo ni lahaja ya Kimvita.
Katika muktadha huu, jumbe hizo zinahitaji fasiri na maelezo
kutokana na utamaduni wa mtunzi. Kwa mapana, mashairi hayo yana
mwangwi unaogusia historia yataifa lake (hasa katika miaka ya baada
ya 1963 nchini Kenya). Kwa maana hii, ushairi wa Abdilatif Abdalla
unaweza kwa kihifadhi na kibainishaji cha vielelelzo vya utamaduni na
uhalisi wa maisha ya jamii ya mtunzi. Katika kushughulikia uhusiano
uliopo kati ya fasihi na utamaduni, makala haya yanaangazia baadhi
ya mifano ya mashairi yaliyohifadhiwa katika Diwani ya Sauti ya
Dhiki (1973). Mwishowe, inapependekeza namna mashari teule ya
Kiswahili yanavyoweza kuwa hifadhi ya ‘viashiria’ vya ‘viishara’
vyatamaduni asilia katika jamii ya sasa.
Description
This paper examines the poetry of Abdilatif Abdalla to determine the
way in which social cultural issues of the Swahili people are presented.
The issues relate to the way in which the people integrate and deal
with their life affairs. In addition, the identification of the social
cultural issues is based on how the poet, as a member of Swahili
society, deals with them. The results show that figurative language,
especially the Kimvita dialect, is used to hide the poet’s feelings.
Therefore, the poet’s culture needs to be taken into account in the effort
to unravel his messages. Generally, his poetry mirrors the history of his
nation (since the years after Kenya’s independence in 1963). Thus, the
poetry of Abdilatif Abdalla can be a treasure trove of the culture and life of his people. In examining the relationship between literature and culture, this paper analyzes some of the poems in the anthology entitled
“Diwani ya Sauti ya Dhiki” (1973). Finally, it makes recommendations
as to how peoms written in Kiswahili can preserve the people’s real
culture in the present society
Keywords
Mashairi, Abdilatif Abdalla, Utamaduni, Waswahili, Mtunzi, Viashiria, Uhalisi, Viishara