Ushairi wa Abdilatif Abdalla Katika Kubainisha Utamaduni wa Waswahili

Thumbnail Image

Date

2018

Authors

Maitaria, Joseph Nyehita
Wafula, Richard Makhanu

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

Journal of Linguistics and Language in Education

Abstract

Makala haya yanafafanua maudhui yaliyomo katika tungo za mashairi ya Abdilatif Abdalla kwa kuzingatia namna masuala ya utamaduni waWaswahili yanavyowasilishwa. Masuala hayo yanahusu namna wenyeji hao wanavyotangamana na wanavyoshughulikia maisha yao kwa ujumla. Kadhalika, ubainishaji wa vipengele hivyo vimewasilishwa kwa kuzingatia taijriba ya mtunzi kama mmoja katika jamii hiyo. Mashairi hayo yanapozingatiwa, inabainika kuwa; hisi za mtunzi zimedhibitiwa kwa lugha teule ya mafumbo inayojikita katika zaidi katika ‘lugha’ au ‘lafudhi’ yake ambayo ni lahaja ya Kimvita. Katika muktadha huu, jumbe hizo zinahitaji fasiri na maelezo kutokana na utamaduni wa mtunzi. Kwa mapana, mashairi hayo yana mwangwi unaogusia historia yataifa lake (hasa katika miaka ya baada ya 1963 nchini Kenya). Kwa maana hii, ushairi wa Abdilatif Abdalla unaweza kwa kihifadhi na kibainishaji cha vielelelzo vya utamaduni na uhalisi wa maisha ya jamii ya mtunzi. Katika kushughulikia uhusiano uliopo kati ya fasihi na utamaduni, makala haya yanaangazia baadhi ya mifano ya mashairi yaliyohifadhiwa katika Diwani ya Sauti ya Dhiki (1973). Mwishowe, inapependekeza namna mashari teule ya Kiswahili yanavyoweza kuwa hifadhi ya ‘viashiria’ vya ‘viishara’ vyatamaduni asilia katika jamii ya sasa.

Description

This paper examines the poetry of Abdilatif Abdalla to determine the way in which social cultural issues of the Swahili people are presented. The issues relate to the way in which the people integrate and deal with their life affairs. In addition, the identification of the social cultural issues is based on how the poet, as a member of Swahili society, deals with them. The results show that figurative language, especially the Kimvita dialect, is used to hide the poet’s feelings. Therefore, the poet’s culture needs to be taken into account in the effort to unravel his messages. Generally, his poetry mirrors the history of his nation (since the years after Kenya’s independence in 1963). Thus, the poetry of Abdilatif Abdalla can be a treasure trove of the culture and life of his people. In examining the relationship between literature and culture, this paper analyzes some of the poems in the anthology entitled “Diwani ya Sauti ya Dhiki” (1973). Finally, it makes recommendations as to how peoms written in Kiswahili can preserve the people’s real culture in the present society

Keywords

Mashairi, Abdilatif Abdalla, Utamaduni, Waswahili, Mtunzi, Viashiria, Uhalisi, Viishara

Citation

Endorsement

Review

Supplemented By

Referenced By