• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Research Papers
    • School of Education and Social sciences
    • Department of Humanities and Languages
    • View Item
    •   Repository Home
    • Research Papers
    • School of Education and Social sciences
    • Department of Humanities and Languages
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Hadhira ya ushairi huru wa Kiswahili ni ipi ?

    Thumbnail
    View/Open
    Full-text (484.7Kb)
    Date
    2021-10-20
    Author
    Maitaria, Joseph
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Makala hii inaangazia mustakabali wa hadhira katika upokezi wa ushairi huru wa Kiswahili. Mwanzoni mwa miaka 1970, ushairi huu ulijitokeza kwa kasi na ulituhumiwa kwa kutozingatia arudhi za kimapokeo. Watunzi wa awali wa ushairi huu walikuwa wataalamu wa lugha na wahakiki wa fasihi; waliotoa maelezo muhimu kuhusu dhana na sifa za ushairi wa Kiswahili. Kabla ya miaka 1960, ushairi wa kimapokeo ulikuwa umesambaa na umezoewa katika jamii. Kujitokeza kwa ushairi huru kulisababisha watunzi na hadhira kugawanyika katika makundi: lile linalojinasibisha na arudhi, lile lisilojinasibisha na arudhi, na lile linalojinasibisha kwa kiasi na arudhi hizo. Katika miaka ya 1970, waliouendeleza zaidi ushairi huru walikuwa ‘vijana’ waliobahatika kupata elimu ya juu katika taaluma ya fasihi na walitarajia kuchangia katika ufafanuzi wa dhana na sifa za ushairi wa Kiswahili kwa ujumla. Swali linalofafanuliwa katika makala hii ni: kwa nini ushairi huru wa Kiswahili ni kivutio cha wataalamu wa lugha na wahakiki wa fasihi? Nadharia ya Semiotiki imetumika kufafanulia matini za lugha kama viishara na viashiria vinavyohitaji kufasiriwa. Data ya uchanganuzi ilitokana na upitiaji wa mashairi katika diwani teule za mashairi ya Kiswahili. Aidha, data nyingine ilitokana na usaili na hojaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na wataalamu wa lugha na fasihi.
    URI
    https://karuspace.karu.ac.ke/handle/20.500.12092/2516
    Collections
    • Department of Humanities and Languages [47]

    Karatina University copyright © 2017-2019  | Powered by DSpace
    Contact Us | Send Feedback | OAI-PMH Compliant
    Theme by Systems Librarian
      

     

    Browse

    All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Statistics

    View Usage Statistics

    Karatina University copyright © 2017-2019  | Powered by DSpace
    Contact Us | Send Feedback | OAI-PMH Compliant
    Theme by Systems Librarian